Namskurum
Mungu kama Mkurugenzi wa Rumafrica (Rulea
Sanga) kwa kupata kibali cha kuhudhuria ibada ya Jumapili 16.12.2012 katika
kanisa la Efatha la Nabii na Mtume Josephate Mwingira. Imekuwa baraka kwangu
kutokana na mafundisho yaliyokuwa yanaendelea mahali pale. Nimepata kujua maana
ya imani na faida zake. Ni hakika kama utasoma
yale yote niliyokuletea naamini yataenda kufanyika baraka katika maisha yako.
Na hivi ndivyo ilivyokuwa:
Rulea akitafakari Neno la Mungu lililohubiria siku ya Jumapili ofisini kwake baada ya kurudi tokea kanisani.

Rulea akitafakari Neno la Mungu lililohubiria siku ya Jumapili ofisini kwake baada ya kurudi tokea kanisani.
HAKIKISHA
UNAYEMWAMINI YUKO HAI AU AMEKUFA?
Naomba
tusome Warumi 10:17. Wiki iliyopita tulijifunza nini maana ya imani? Na
inafanya kazi gani?
IMANI
chanzo chake ni kusikia na kusikia huja kwa Neno la Kristo. Kuna watu wamesikia
habari za mtume Fulani na kujenga imani yao
kwake, na wengine wamesikia habari za makaburini na kujenga imani huko. Ili uonekane umeokoka, lazima uwe na imani, kwasababu
huwakilisha kuwa huyu anaelewa nini na anajua nini?
Tusome tena
Waebrania 11:1-6. Imani ni kuwa na uhakika wa mambo yatarajiwayo, ni bayana ya
mambo yasio onekana. Mungu anapoaanza kusikia Neno huwa ana imani na kuamini
lile Neno.
Kuwa
mwangalifu sana
ma I,ani unayotembea nayo kwasbabu unaweza kuwa na uhakika na kitu kilichoharibika.
Imani ni mtu amabye anahakika na jambo kuwa hili jambo linaenda kutendeka na
unaenda kupata.
Imani haioni kitu ambacho hakionekani, bali huona kitu ambacho kinaonekana na hakipo. Mtu anayepaswa kuwa na uhakika wa mambo ni wewe na mimi tuliyeokoka. Imani inakuja kwa kusikia, Je, unasikia kushinda au kushindwa? Kama unasikia kushinda utashinda na kama unasikia kushindwa utashindwa. Kama ulisikia kwamba ndugu zako ni maskini na wewe utakuwa maskini, na akaamini, tambua hilo linaenda kufanyika kwasababu umesikia na umeamini.
Imani haioni kitu ambacho hakionekani, bali huona kitu ambacho kinaonekana na hakipo. Mtu anayepaswa kuwa na uhakika wa mambo ni wewe na mimi tuliyeokoka. Imani inakuja kwa kusikia, Je, unasikia kushinda au kushindwa? Kama unasikia kushinda utashinda na kama unasikia kushindwa utashindwa. Kama ulisikia kwamba ndugu zako ni maskini na wewe utakuwa maskini, na akaamini, tambua hilo linaenda kufanyika kwasababu umesikia na umeamini.
Imani
imejengwa kwa msingi wa Mungu. Mungu haonekani kwa macho lakini unasikia kuwa
yuko Mungu na ndio maana up oleo kanisani na unamaamini hivyo hata kama hujawahi kumuona kwa macho yako.
Tunashinda mambo yetu kwasababu tunaimani kuwa Mungu atatushindia. Imani uliyonayo wewe ina nguvu na hakuna mafuriko au upepo utakaoondoa imani yako kwasababu imejengwa katika mwamba wa yesu Kristo..
Tunashinda mambo yetu kwasababu tunaimani kuwa Mungu atatushindia. Imani uliyonayo wewe ina nguvu na hakuna mafuriko au upepo utakaoondoa imani yako kwasababu imejengwa katika mwamba wa yesu Kristo..
Watu wengi
wanafanya vituko vingi kama vile ufisadi
wakiaamini ni nguvu zao. Kumbuka chochote unachofanya duniani ipo siku utatoa
hesabu. Hakuna aliyeko duniani kwa bahati mbaya, jua Mungu anampango na wewe na
anataka akutumie katika kazi yake.
Tunaokoka
kwasababu tunampenda Mungu na sio kwa matendo mazuri tunayofanya, na pia imani
yetu inatuhakikishia kuwa tuko na Mungu.
Imani
haitaji kuwa na imani kubwa, ila ukisikia na ukakubali kwa kusikia kwako
utashinda yale yanayokuzunguka. Imani tunayoongelea ni ya Mungu na sio imani
zingine za kipagani na mashetani.
Imani
inachukua vitu vilivyosirini na kuweka wazi. Imani hii ikiwa imemwamni Mungu,
imani inaenda kwa Mungu na kujenga uhusiano, na uhusiano huo unakuja kwetu
kwasababu tunamwamini.
Umimwamini
Yesu atakupa uzima wa milele. Mtu mwenye imani hana hofu. Imani tuliyonayo
inashuhudia kile tulichokiona, inaeleza tulichokiona. Imani yako haitaji kuwa
na mtu mkubwa wa kufundisha ila inahitaji wewe kuichochea hiyo imani yako
ndogo.
Imani ya mtu muda mwingine inasongwa sana. Unachotakiwa ni kupalilia imani yako na kusonga mbele. Linakuja jaribu pambana nalo na sahau na uendelee mbele na imani yako. Jaribu ulilonalo linakusukuma kwenye kusudio. Imani inaweza kukufanya hata adui zako kukufuata na kukutafuta uliko na kukupigia magoti. Unatakiwa kutopoteza imani uliyonayo kwasababu ina thamni sana.
Imani ya mtu muda mwingine inasongwa sana. Unachotakiwa ni kupalilia imani yako na kusonga mbele. Linakuja jaribu pambana nalo na sahau na uendelee mbele na imani yako. Jaribu ulilonalo linakusukuma kwenye kusudio. Imani inaweza kukufanya hata adui zako kukufuata na kukutafuta uliko na kukupigia magoti. Unatakiwa kutopoteza imani uliyonayo kwasababu ina thamni sana.
Wewe mwenye
imani, angalia sana
unachosikia na unapaswa kujua sheria za Mungu. Unapokosa kuwa na imani wakati
wa ugonjwa wako, kitu unachowaza ni kifo kwasababu huna uhakika kuwa Mungu
anaweza kuponya.
Imani
tuliyonayo ina nguvu na inashuhuda. Unapokuwa duniani na kuamni kuwa Yesu
Kristo ni mwokozi wako, amini matatizo yako hayatakusonga tena. Yaliyoandikwa
katika Biblia sio kwaajili ya historia ila ni kwa watu wa Mungu kuamini na
watakachochukua katika Biblia wanenda kupona.
Unapovumilia
mpaka mwish, ndipo unapookoka. Imani yako inatakiwa iwe na ujasiri. Unapoumwa
vumilia na amini kuwa unaenda kupona. Imani alzima iwe na ujasiri ili uweze
kushinda kwasbabu imani yetu ina mapmbano, kuna watu wanataka ushindwe..
Imani yako
imejengwa kwenye Neno la Mungu ambalo ni sheria ya Mungu ambayo unatakiwa
kufuata. Kila mtu aliyekuwepo hapa duniani awe ameokoka au hajaokoka lazima
afuate sheria ya Mungu kutoka katika Biblia. Mungu anapoona ufuuati sheria
ndipo unapoanza kupata mateso.
Huhitaji
kuwa na imani kubwa sana
bali kuwa na ujasiri wa imani yako kwasababu imani inakua na kuongezeka. Imani
inakua na utukufu hadi utukufu. Kila unapoendelea kupanda ngazi, kuna jaribu
utapitia.
Imani
inakupa kufahamu yaliyokuzunguka na unakoendea. Imani inakusaidia kufahamu
ulipo na unakoenda. Tunafahamu ya kuwa ulimwengu uliumbwa kwasbabu tunaimani
kutokana na maneno ya Mungu tuliyosikia na kuambiwa. Imani yako inakusaidia
kufahamu kuwa wewe hakuna atakayekusumbua. Tambua ya kuwa aliyeokoka analindwa
na yuko ndani ya Kristo.
Ukiwa na Kristo hakuna utakachopungukiwa. Lakini kuna jambo la kujiuliza, kwanini wewe unasema unaye kristo na shetani anakutawala? Ukiwa na imani unakuwa makini na mwendo wako. Imani sio kitu cha kuchezea, shetani anakuja kwako sio kwasbabu ni mzuri sana wa sura iala ni kutokana na imani yako. Mtu anapona kwasbabu ana imani. Yesu alipokuwa anawaombea wagonjwa alisema” Imani yako imekuponya, usitende dhambi tena” Dhambi zetu ndizo zinatutesa.
Ukiwa na Kristo hakuna utakachopungukiwa. Lakini kuna jambo la kujiuliza, kwanini wewe unasema unaye kristo na shetani anakutawala? Ukiwa na imani unakuwa makini na mwendo wako. Imani sio kitu cha kuchezea, shetani anakuja kwako sio kwasbabu ni mzuri sana wa sura iala ni kutokana na imani yako. Mtu anapona kwasbabu ana imani. Yesu alipokuwa anawaombea wagonjwa alisema” Imani yako imekuponya, usitende dhambi tena” Dhambi zetu ndizo zinatutesa.
Imani haiku
mbinguni ila iko kwako. Yeyote aliyeokoka yupo pale Yesu yupo, ambapo imani
imekaa.
Mungu ukiwa
naye hakuna atakayekuondoa chini. Ya jua hili kwasababu sisi sote tunalindwa
kwa nguvu za Mungu. Unapokosea na kupatwa na matatizo ujue Mungu anakuchapa
kwasababu umempoteza. Mungu anapokuchapa anakurudisha kwake kwasbabu anaona
umepotea na unaenda kubaya zaidi.
Unapookoka
unakuwa unasababisha matakataka kuoshwa upya. Unapokua kanisani usiwe
unakuja kama desturi ila umekuja ili aondoe jambo linalokusumbua.
Imani
inafanya vitu kuwa na ubora na haifanyi ovyo ovyo kwasababu yule aliye na asali
ya Imani bora ni bora. Ili ufanye vitu vyenye
ubora lazima uwe na imani ya kumpendeza Mungu. Imani ni kutafuta kwa kuleta vya
sirini kuwa dhahiri.
Wale
wamtafutao Bwana kwa imani atawapa utajiri ambao una furaha na kicheko. Munu aliyetuumba
anataka watu wake kuishi maisha ya furaha na amani. Ukiwa na pesa mtafute Yesu
kwa bidii. Wewe uliyeamuna kuwa na Yesu tegemea kuwa dhawabu.
Ulipookoka
ulisema Mungu atakubariki, na umekaa mika miwili na umeona hakuna kubarikiwa na
unatamani kuacha, nakuambia endelea kuchochea imani yako. Imani mara nyingi
inaenda na maamuzi, nje ya maamuzi imani haiendi kufanya kazi.
Mungu amekuwa mwema kwako kutokana na imani yako yenye maamuzi na maamuzi ya kusaidia imani yako kutoyumba, kwa na ujasiri na kuwa na nguvu. Imani yako haitakiwi kuyumbishwa. Imani na maamuzi ni mwamba imara, haikupi kuona uharibifu ila kufajhamu kuleta kilicho bora siku zote
Mungu amekuwa mwema kwako kutokana na imani yako yenye maamuzi na maamuzi ya kusaidia imani yako kutoyumba, kwa na ujasiri na kuwa na nguvu. Imani yako haitakiwi kuyumbishwa. Imani na maamuzi ni mwamba imara, haikupi kuona uharibifu ila kufajhamu kuleta kilicho bora siku zote
MUNGU
AKUBARIKI
Rulea Sanga
Mkurugenzi wa Rumafrica
+255 715 851523
No comments:
Post a Comment