Jumapili hii kulikuwa na maombezi kwa mama wajawazito, waliokoka, na watu wenye shida mbalimbali.
SALAMU KUTOKA KWA MRS. NABII NA MTUME JOSEPHATE MWINGIRA.
Mungu wa Efatha anatushangaza, ukimtumikia utaona matunda yake. Tusome Zaburi 95:1-6, Njoo tumwimbie BWANA, tumfanyie shangwe mwamba wa wokovu wetu. Tuje mbele zake kwa shukrani, tumfanyie shangwe kwa zaburi, kwa kuwa BWANA ni Mungu na mkuu, na mfalme mkuu juu ya miungu yote. Mokononi mwake zimo bonde za dunia, hata vilele vya milima ni vyake. Bahari ni yake, ndiye aliyeifanya, na mikono yake iliumba nchi kavu. Njoo tuabudu, tusujudu, tupige magoti mbele za BWANA aliyetuumba.
Twende kwa Bwana na shukrani. Tatizo hata likiwa kubwa kwako litaenda kupungua kwani liko jina lenye nguvu (Yesu Kristo) wewe unatakiwa kuamini tu. Ubatakiwa kubadilika na kuwa na tabia mpya kwani ulipookoka uliachana na tabia mbaya na sasa uko katika himaya ya Yesu ya kuwa na tabia kama Zake.
Jinsi
unavyotamka ndivyo unavyokuwa. Kwahiyo maneno yako yanaweza kuumba tabia Fulani
maisha mwako. Kama wewe unatamka mema tu basi utakuwa mwema na kama unatamka na kufikiria mabaya utakuwa na matendo
mabaya na mwisho wake ni mbaya.
Jizoeshe
kuwa mtu wa shukrani kwa kile Mungu anakupa kwa siku na siku zote za maisha
yako. Unapoenda mbele za Mungu toa sadaka yenye harufu nzuri mbele zake. Fungu
lako ni agizo, kwahiyo huruhusiwi kula fungu la kumi.
TANGAZO LA MKESHA IJUMAA
Kabla
hatujasoma Neno la Mungu, ningependa kuwajulisha yakuwa Ijumaa ni siku ya
mkesha, kila mmoja akae mbele za Mungu
na andaa moyo wako kukesha na Bwana.
TAARIFA ZA UGENI ULIOFIKA EFATHA
Pia ningependa kuwajulisha kuwa leo kanisani kwetu tumetembelewa na wachungaji wengi sana kutoka Tanzania na nje ya Tanzania wamekuja kwaajili ya kushangilia na sisi katika kipindi hiki cha mashangilio. Siku ya leo ni siku ya mashangilio, na Yesu ametutangulia na kuwahi kanisani kabla yetu, kwa maana siku zote Yesu huwa anachelewa kidogo na sisi tunakuwa watu wa kumkaribisha.
TAARIFA ZA UGENI ULIOFIKA EFATHA
Pia ningependa kuwajulisha kuwa leo kanisani kwetu tumetembelewa na wachungaji wengi sana kutoka Tanzania na nje ya Tanzania wamekuja kwaajili ya kushangilia na sisi katika kipindi hiki cha mashangilio. Siku ya leo ni siku ya mashangilio, na Yesu ametutangulia na kuwahi kanisani kabla yetu, kwa maana siku zote Yesu huwa anachelewa kidogo na sisi tunakuwa watu wa kumkaribisha.
SHUHUDA
Leo kuna
mtoto wa kiume amezaliwa kanisani. Mama huyu alipata uchungu tokea Jumanne na
akaenda hospitalini na kuambia atafanyiwa operationa (atajifungua kwa kisu). Mama
huyu alikataa ushauri wa daktari na kuamua kuja kanisani Efatha. Alipofika hapa
yalifanyika maombi. Baada ya maombi kuisha mama alijifungua mtoto wa kilo tatu
na nusu kanisani kwa njia salama. Alipoingilia mtoto ndipo alipotokea.
Tuunamshukuru Mungu.
Ninachotaka
kuwaambia kuna siku watu watazaa humu kanisani na mtashangaa vitoto vikilialia.
Siku moja
Yesu alipotoka safari kuelekea Yerusalemu, alisema “Mtamuona mwana punda
mfungueni na mkiulizwa, semeni, Bwana anamhitaji” Hata wewe ukiona mtu
amefungwa basi unatakiwa kumfungua na ukiulizwa, sema Bwana anamhitaji. Mkiona
mtu anauhitaji, mpeni na msiwe wanyimi. Nimemuomba Bwana atoe kile kilicho
chake na awape ninyi wenye uhitaji..Pokea kwa jina la Yesu!!!. Na kile
nilichonacho Nabii wenu Mungu akupe na wewe kwa jina la Yesu.
Nimemuomba
Mungu anipe wenye Roho ya Efatha, wale wenye uhitaji wa kumtafuta Mungu kwa
akili zao na mali
zao.
MAONO
Nabii na Mtumwa Josephate Mwingira alimuona mtu mwenye mateso katika ulimwengu wa Kiroho na alipomuita kwa jina yule mama alijitokeza huku akilia machozi, kwani hakutegemea kabisa kuitwa. Na hivi ndivyo alivyosema
MAONO
Nabii na Mtumwa Josephate Mwingira alimuona mtu mwenye mateso katika ulimwengu wa Kiroho na alipomuita kwa jina yule mama alijitokeza huku akilia machozi, kwani hakutegemea kabisa kuitwa. Na hivi ndivyo alivyosema
Kuna mama
mmoja anaitwa Maria John, nasikia sauti hii kutoka mbinguni ikiita. Sasa unaondolewa
na mizigo yako. Nakuomba uje mbele haraka sana.
Na wewe unayekandamizwa uondolewe na mikandamizo yako.
Kuna wakati
Mungu anashughulika na watu bila ya wewe kujua. Unaweza kuona mtu anafanikiwa
na hujui ni kitu gani kinamfanya huyu mtu afanikiwe, ila Mungu peke yalke ndiye
anayejua.
Kanisani ni
mahali pa kukaa na watakatifu bna sio na wenye mapepo. Mapepo hukaa kwa wanyama
hasa nguruwe, kwahiyo mapepo kama mpo kanisani
nawaamuru kuondoka na mkaishi katika sehemu zenu chafu.
SOMO LA
JUMAPILI KUTOKA KWA NABII NA MTUME JOSEPHATE MWINGIRA.
“ROHO WA
BWANA YU JUU YANGU”
Tusome Luka 4:18, Roho wa Bwana yu juu yangu, kwa maana amenitia mafuta kuwahubiria maskini habari njema. Amenituma kuwatangazia wafungwa kufunguliwa kwao, vipofu kupata kuona tena, kuwaacha huru waliosetwa, na kutangaza mwaka wa Bwana uliokubariwa.
Tusome Luka 4:18, Roho wa Bwana yu juu yangu, kwa maana amenitia mafuta kuwahubiria maskini habari njema. Amenituma kuwatangazia wafungwa kufunguliwa kwao, vipofu kupata kuona tena, kuwaacha huru waliosetwa, na kutangaza mwaka wa Bwana uliokubariwa.
Roho wa Bwana
yu juu yangu kwasababu amenitia mafuta ya furaha. Wakati wengine wanabarikiwa,
mimi lazima nibarikiwa zaidi yao
kidogo. Mungu anasema hamtakuwa mkia bali vichwa, na wewe utakuwa unapokea na
kuwapa watu wengine.
Mwisho
nasema, naomba ukae mbali na dhambi kwani utaona mashangilio. Mwamini Mungu
kwani mwaka huu ni mwaka wa mashangilio.
MUNGU
AWABARIKI
Mwandishi
Rulea Sanga
No comments:
Post a Comment