ROHO WA
BWANA YU JUU YANGU
Ukiwa
umeokoka uwe mmoja wa watendaji na usiwe mtu wa kuchungulia na kushangaa
wenzako wanaofanya kazi ya Mungu, jihusishe kwa kufanya kazi ya Mungu kwa
vitendo na usiwe mtu wa kupokea tu. Kama wewe ni mwimbaji basi imba sana, kama wewe unahusika na mitandao basi sambaza Neno la
Mungu, kama wewe ni mchungaji fanya kazi ya Bwana kama
hutakuja kufanya tena n.k.

Roho wa
Bwana yu juu yangu kwasababu Bwana amenipaka mafuta ya furaha. Mwaka huu ni
mwaka wa mashangilio na kila siku ni shangwe.
MACHO KUONA
TENA.
Ili
macho kuona tena kuna mambo ya kuzingatia ambapo Neno linaeleza kuna mambo
unayahitaji:
MOJA:
(Yohana 1:3). Neno linakusaidia kuona. Unatakiwa kutenga muda wako kwa siku na
kutafuta sehemu tlivu na anza kusoma Neno la Mungu na kuomba kwa muda wa siku
kama nne.
Ukiomba
jambo lolote lolote kwa Baba na Yeye atalifanya, ili BABA atukuzwe
(Yohana 14:13).
Kila aminiye Mimi nia kazi ninazozifanya na yeye atafanya zaidi. Yangu, na kila
anachokiomba kwa jina langu, Mungu atafanya na jina la Bwana litatukuzwa.
Pata nafasi
ya kutulia na kupata Neno, na katika Neno kuna chakula cha uzima. (Yohana
6:32), hata kama umechoka kimwili, nenda
kusoma Neno la Mungu na ukifanya hivyo mwili wako unahuwishwa na unatiwa nguvu
ya kusoma Neno la Mungu na kusonga mbele.
(Timotheo
2:3), Neno ni pumzi ya Mungu na hutuongoza, hutuadisha ili watu wa Mungu wawe
kamili. Kwahiyo tunaweza kusema Neno la Mungu linafanya yafuatayo
(a)
Linakuongoza
(b)
Linakuadibisha
(c)
Linakukamilisha
Ili
mtu awe kamili, amekamilishwa kutenda mema. Unatakiwa kuwa mwema mpaka jirani
yako aone kweli umeokoka. Na sio matendo yako machoni pa watu ni vituko na wanabaki
wanashangaa kuwa huyu kweli amekoka!!
Katika
shida unayopitia, kibu lake
liko kwenye andiko,
haupaswi kupata shida juu ya shida yako unayopitia. Wewe soma neno la Mungu na
mwisho wa siku utapata jibu la shida yako.
Waume
mnapaswa kuwapenda sana wake zenu kama Yesu alivyoupenda ulimwengu na akafa ili mimi na
wewe tupone. Miwanyanyase wake zenu kwani hao ndio waliokufanya mpaka sasa
unaonekana hivyo. Kama mama yako angekuwa
hakupendi,hangeweza kukuzaa, lakini aliamua kukaa na wewe mpaka ukazaliwa.
Kabla
maumivu au jambo lolote halijafika angalia Neno. Unaweza kutambua jema kama una Neno la Mungu. Neno la Mungu linakupa mwisho wa
jambo kuwa mwema na kukupa ushangilio.
Magonjwa na
maumivu mengi yanaletwa kama huna Neno.
Unapokuwa na Neno la Mungu linakukinga na wale wabaya wanaoweza kusababisha
magonjwa kwako. Kila watakapotaka kukuingilia wanakutana na ulinzi wa Neno.
(Timotji
2:4:6-7), Hufi ghafla, bali unaaga na kutangaza kifo mapema. Kifo cha mwamini
si cha ghafla ila unapata muda wa kuagana na wenzako. Yesu aliumaliza mwendo
na hakuishi njiani. Kuna watu wengine
hapa kanisani Efatha tunawapa Uaskofu na wakipata baada ya muda wanaacha nap
engine kuhama kanisani. Ukipewa kazi ya Mungu fanya kwa uaminifu mpaka mwisho
wa mwendo ili ukabidhi kwa ushindi.
Unapoenda
kusoma Biblia unaendelea kulinda imani yako. Mtu mwenye Imani hawezi kuliwa na
shetani na shetani hawezi kumsumbua. Kama una
nguvu ya Mungu huhitaji kulia ila mshukuru Mungu na kumuombea mmbaya wako
anayekujia.
Maumivu na
mateso mnayoyapata ni kwasababu hamfuati maelekezo ya Mungu mnayoambiwa na
watumishi wenu na yaliyomo katika kitabu Kitakatifu yaani Biblia.
Neno la
Mungu linakupa ujasiri wa kuomba. Kitu cha muhimu sio ushuhuda ila mtu kupata
kuokoka. Yesu hakuja kwaajili ya wagonjwa ila alikuja kuwaokoa. Makuhani waliponya
ila hawakuwaokoa watu mpaka Yesu alipokuja. Unatakiwa kujiuliza, umesababisha
wangapi kuokoka..?
(Yohana
1;5:14-15), ndani ya Neno unapata ujasiri wa kitu unachosema. Neno linasema
ukiomba lolote kwa jina la Langu, mimi Bwana nitatenda. Neno la Mungu linakupa
yale akukarimiaye.
(Wakoritho
1:2:12), ukiangalia Neno ndipo unajua nini Mungu amekukeremea. Mungu hajibu
maombi yasio na Neno lake. Omba kulingana na neno la Mungu. Mungu haangali
umaskini wa mtu bali anaangalia moyo wake unaohitaji utajiri. Mungu anaangalia mambo
yafuatayo huko ndani ya moyo wako ili akupe utajiri:
(a)
Kusudi la Mungu. Ukipata utajiri utakuwa na kusudi gani mbele za Mungu?
(b)
Utafanya kazi ya Mungu. Kama utapewa
huo utajiri, utafanya kazi ya Mungu au ni kwaajili ya mahitaji yako nay a familia
yako?
(c)
Unaupendo wa Mungu. Ukipata huo utajiri utazidi kuwa na upendo wa Mungu,
au ndo kwanza utawachukia wenzako pamoja na kupuuzia kazi ya Mungu?
(d)
Matumizi yako ya kila siku. Je, matumizi yako yataendana nay ale ya
Mungu?
Mungu
anaangalia Neno linasemaje huko ndani yako. Unaongea ubinafsi wako au ukuu wa
Mungu?
No comments:
Post a Comment